Friday, May 18, 2007

KAULI YA JAJI MKUU SAMATA IWE CHANGAMOTO KWA WADAU WA SHERIA NCHINI



Katika mamabo ambayo watanzania tumekua tukijigamba na kutembea vifua mbele ni AMANI iliyotawala nchini tangu tulipopata uhuru karibu miongo minne na nusu iliyopita..Nchi yetu imetokea kua kimbilio la wageni kutoka nchi majirani ambapo hapakaliki kutokana na kutoelewana na vita vya wenyewe kwa wenyewe na vita vya kimakundi au kimatabaka kati ya watawala na wananchi wao.


Sina haja ya kuingia kwa undani katika hali tete inayoendelea kwa majirani zetu ila kwa kuanzia mada iliyobeba kichwa cha habari hapo juu niliona ni busara kugusua kwa uchache maswahibu yanayowakumba wenzetu katika siasa zao na mifumo ya utawala na ya kutetetea haki zao.


Jana Mheshimiwa jaji mkuu Barnabas Samatta aligusia juu ya umuhimu wa vyombo vya sheria hasa mahakama katika kudumisha amani ya nchi husika kwa kuweka bayana kua...nanukuu "Iwapo jamii itapoteza imani kwa mahakama zetu ndio itakua mwanzo wa kupoteza amani nchini" Inawezekana ikaonekana ni sentensi fupi na iliyozoeleka lakini suala linabaki kua ni jitihada zipi zimefanyika katika kunusuru hali hiyo isitokee???Tunafanya nini ili kuhakikisha wananchi wetu hasa wale waliokata tamaa hawapotezi imani kwa vyombo vyetu hivi ambavyo ni mhimili muhimu katika utawala wa kidemokrasia na wenye kuheshimu haki za binadamu????


Kauli hii imekuja wakati muafaka wakati kukiwa na malalamiko mengi juu ya ubabaishaji unaofanywa na vyombo hivi katika kutetea haki za wanyonge.....Kumekua na ucheleweshaji wa kesi katika kiwango cha kukatisha tamaa na hata mara nyingine kutolewa maamuzi ambayo wakati mwingine yamekua yakizua mjadala juu ya umakini wa vyombo vyetu hivi..Sina nia ya kubeza kila jema linalofanywa na na mahakama zetu ila ni katika kuleta changamoto kwenye mchakato wa wadau kuelekea kwenye ujenzi wa jamii wenye kuheshimu haki za wananchi wenzetu..


Kumekua na migogoro mingi kati ya mtu na mtu,jamii na jamii,wananchi na serikali,wafanyakazi na waajiri wao,wanafunzi na uongozi wao lakini je "nii hatma ya kelele na tofauti zitokanazo na misuguano ya makundi hayo"?? Siku zote binadamu amekua na tabia ya kujaribu njia mbadala pale anapoona nia na mitazamo yao haiendi sawa na kama walivyotaraji....vitendo vya kuchoma vibaka moto ni kielelezo kirahisi cha kuelezea kuchoshwa na ufanisi wa baadhi ya taasisi au asasi zilizokabidhiwa majukumu ya kusimamia mambo kama hayo....Kwanini raia ambaye amechoshwa na tabia ya jambazi sugu au vibaka wazoefu asiamue kuchukua sheria mkononi wakati kila wanapopoleka malalamiko yao kwenye vyombo husika,hakuna maamuzi ambayo yataonekana kukidhi kero za walalamikaji!!!!!!


Kuna kesi nyingi katika sekta ya madini kati ya wachimbaji wadogo wadogo na wamiliki wa makampuni ya kigeni,kuna kesi nyingi kati ya wafanyakazi na waajiri wao ambazo bado mwisho wake haujulikani,wastaafu kila siku wanatanga na njia katika kufuatilia haki zao lakini bila matumaini yoyote katika yale mambo wanayodai ambayo asilimia 90% ni ya msingi!!!!!! Siku za karibuni kumekua na zoezi la bomoa bomoa katika jiji la Dar Es Salaam na asilimia kubwa ya wahanga wa tatizo hilo ni machinga.....vibanda vyao vingi vilipitiwa na sulubu hiyo...Sina nia ya kubeza zoezi hilo kwani mantiki yake iko wazi kabisa 'Kupendezesha mandhari ya jiji' hili ni jambo jema na linapaswa kupongezwa na kila mtu lakini swali la msingi ambalo linastaajabisha kila watu makini ni "Kwanini baadhi ya vibanda viachwe" Katika gazeti tando la michuzi alipiga picha ya moja ya vibanda hivyo na kuhoji uhalali wa kuwepo kwake????Watu wengi walichangia na kusema pengine ni cha mkubwa flani!!!je wakubwa hawapaswi kuguswa na sheria????je hao ndo wanapaswa kua juu ya sheria????


Iko mifano mingi ambayo inatia kichefuchefu katika utekelezaji wa mambo ambayo ni ya manufaa kwa wananchi...Nani hajui kua karibu asilimia 60 ya vituo vya mafuta vilivyopo katika jiji la Dar Es Salaam vipo kinyume na sheria???Je wasimamizi wa sheria hizo wako wapi??? au tunataka wananchi waanze kuamini kua hizo ni miradi ya watunga sera na sheria ambao pia wamepewa ruhusa ya kuzivunja???Ni kwanini majibu ya maswali haya yasipatiwe ufumbuzi wa haraka katika kurudisha imani ya wananchi kwa watawala wao?????


Kwa kumalizia napenda kutoa tu changamoto kwa serikali yetu kua makini katika kusimamia na kutatua kero za wananchi wake ili waendelee kua tayari katika kushiriki kikamilifu utekelezaji wa mipango ya maendeleo yao....Naamini kubwa na serikali ya mheshimiwa baba JK kwahiyo chondechonde watendaji msimwangushe katika nia yake njema ya kujenga nchi moja inayoheshimu haki na yenye kuweka mazingira ya kila mmoja kufaidi matunda ya uhuru...Ubabe wa baadhi ya watendaji hayana nafasi kwasasa kwani mwisho wake hautupi matumaini yoyote mazuri.....Mfano mzuri tunao kwa migomo inayoendelea kwa wanafunzi wa elimu ya juu....hii kwangu ni ishara ya kuchoshwa na ubabaishaji wa baadhi ya watendaji.....Nadhani itabidi tuanze kujadili nia ya mtu kama Proffessor msola katika kutumikia wananchi wa jamuhuri yetu hii.....Inatia hasira pale unaposikia WAZIRI flani msomi anawakatia simu wananchi wake eti kwasababu amechoshwa na kero zao!!!!!!!Hili naomba niliongelee siku nyingine...


Naomba kuwasilisha..