Tuesday, March 30, 2010

SAKATA LA EPA, NI JARIBIO KWA SERIKALI INAYOJIGAMMBA KUFUATA NA KUHESHIMU UTAWALA WA SHERIA.

Katika mambo ambayo watanzania tumekua tukijigamba na kutembea vifua mbele ni AMANI
iliyotawala nchini tangu tulipopata uhuru karibu miongo minne na nusu iliyopita..Nchi yetu imetokea kua kimbilio la wageni kutoka nchi majirani amani kwao imekua ni ndoto kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe au misuguano ya kimakundi au kimatabaka kati ya watawala na wananchi wao au kati ya makundi mbalimbali ya kijamii hasa ya wale walionancho na wasionacho na wale wasiotarajia kuwa nacho.
Proffesor Shivji amekuwa akiyagawa matabaka hayo katika makundi matatu, Walalahai, walalaheri na walalahoi. Sina haja ya kuingia kwa undani katika uahalisia wa maisha ya mtanzania wa kawaida yalivvyo kwani takwimu na mazingira tunayoishi yanajitosheleza kutoa mwanga halisi wa mambo yalivyo na yanavyoendelea kuwa kila kukicha.

Nadhani ni busara kwa watawal wetu kutambua maswahibu yanayowakumba wenzetu wa nchi za jirani mengi yalichangiwa kwa naman mifumo ya siasa katika siasa katika nchi zao zilivyobuniwa na kuendeshwa na namana mifumo ya kutetetea haki za wananchi zinavyoendeshwa.
Jaji mkuu mstaafu Barnabas Samatta alishawahi gusia juu ya umuhimu wa vyombo vya sheria hasa mahakama katika kudumisha amani ya nchi husika kwa kuweka bayana kua...nanukuu "Iwapo jamii itapoteza imani kwa mahakama zetu ndio itakua mwanzo wa kupoteza amani nchini" Inawezekana ikaonekana ni sentensi fupi na iliyozoeleka lakini suala linabaki kua ni jitihada zipi zimefanyika katika kunusuru hali hiyo isitokee???

Tunafanya nini ili kuhakikisha wananchi wetu hasa wale waliokata tamaa hawapotezi imani kwa vyombo vyetu hivi ambavyo ni mhimili muhimu katika utawala wa kidemokrasia na wenye kuheshimu haki za binadamu?Serikali yetu inaziwezesha vipi vyombo hivi tukufu katika kutekeleza majukumu yake matakatifu ya kugawa haki sawa kwa wote?

Nimeamua kurejea kauli ile kwasasa wakati malalamiko yanazidi kua mengi kufuata kigugumizi cha serikali kuwafgikisha wale wahuskia wote katika kashfa ya ufisadi uliofanywa kwenye akaunti ya madeni ya nje(EPA).Wananchi wamepoteza imani kwa serikali yao wakirejea maneno yale yale ya wanyonge siku zote ndio wamekua wakiona upanga wa nguvu za dola na pia menno za mahakama katika utoaji wa haki.

Siku za hivi karibuni,wanasiasa na wananchi wa kawaida wamekua wakishinikiza wafungwa wote walio katika magereza mbali mbali nchini waachiwe huru ikiwa mafisadi waliohusika katika wizi wa mabilioni ya katika benki kuu wachukuliwe hatua stahili.Wakati changamoto hii ikiwa bado haijapata ufumbuzi stahili wananchi wanaanza kuzua wasiwasi mpya kua waliofikishwa mahamakani sio wahusika wakuu katika hilo.Sidhani ni busara kuingia kwa undani katika hilo ila naiachia mahakama jukumu iliyokabidhiwa kwa mujibu wa sheria kuhakikisha haki inatendeka.

Changamoto ni nyingi katika kufuata na kuheshimu utawala wa sheria bila kuangalia historia,cheo au hadhi ya mtu aliyelketwa mbele ya sheria.Kumekua na ucheleweshaji wa kesi katika kiwango cha kukatisha tamaa.Sina nia ya kubeza kila jema linalofanywa na na mahakama zetu na serikali yetu ila ni katika kuleta changamoto kwenye mchakato wa wadau kuelekea kwenye ujenzi wa jamii wenye kuheshimu haki za wananchi wenzetu ni lazima tubuni mfumo imara utakaoleta tija katika kutafuta haki.

Haiingii akilini kwa mtanzania yoyoyote yule kuona nduguye anasota rumande kwa miaka mingi bila shauri lake kupelekwa katika vyombo husika wakati mafisadi na watu wenye hadhi zao wakiwahishwa mahamakamani na misururu mirefu chini ya ulinzi mkali kama msafara wa kiongozi mkuu wa nchi.

Siku zote binadamu amekua na tabia ya kujaribu njia mbadala pale anapoona nia na mitazamo yao haiendi sawa na kama walivyotaraji....vitendo vya kuchoma vibaka moto ni kielelezo kirahisi cha kuelezea kuchoshwa na ufanisi wa baadhi ya taasisi au asasi zilizokabidhiwa majukumu ya kusimamia mambo kama hayo....Kwanini raia ambaye amechoshwa na tabia ya jambazi sugu au vibaka wazoefu asiamue kuchukua sheria mkononi wakati kila wanapopoleka malalamiko yao kwenye vyombo husika,hakuna maamuzi ambayo yataonekana kukidhi kero za walalamikaji!

Sakata la watuhumiwa wa EPA kama serikali na taasisi zake hazitakua makini linaweza kubadil hali ya upepo wa uvumilivu wa wananchi na kuenda mbali zaidi na kuhoji uhalali wa uwepo wa serikali yao ambayo waliiamini na kuipa jukumu la kua msimamizi wa rasilimali zao kwa faida yao wenyewe na kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Kwa kumalizia napenda kutoa changamoto kwa serikali yetu kua makini katika kusimamia na kutatua kero za wananchi wake ili waendelee kua tayari katika kushiriki kikamilifu utekelezaji wa mipango ya maendeleo yao.

Nina imani kubwa na serikali ya mheshimiwa JK kwahiyo chondechonde watendaji msimwangushe katika nia yake njema ya kujenga nchi moja inayoheshimu haki na yenye kuweka mazingira ya kila mmoja kufaidi matunda ya uhuru.

Ni ukweli ulio wazi kua ubabe wa baadhi ya watendaji hauna nafasi kwasasa kwani mwisho wake hautupi matumaini yoyote mazuri.Mfano mzuri tunao kwa migomo inayoendelea kwa wanafunzi wa elimu ya juu,hii ni ishara ya kuchoshwa na ubabaishaji wa baadhi ya watendaji.

Nadhani busara itatendeka katika kutoa haki kwa wanafunzi waliogoma wakishinikiza serikali iyaangalia maombi yao kwa jicho la huruma na sio kukurupuka kutoa adhabu kwa wale ambao siku zote wamekua wakitolewa kafara kama vinara wa migomo ilhali kila mmoja anajua wazi kuwa wao ni wawakilishi wa madai ya msingi yanayotolewa na wenzao wengi ambao wamekua wanataabika katika kutetea haki zao.

Watanzania hawategemei vijana hawa waitwe wahuni kama ambayo waziri alishawahi kuwaita wanafunzi hao wanaharakati wa haki katika taasisi kama chuo kikuu cha Dar Es Salaam.Napata hofu kuwa kama waziri anasema wale wanaogoma katika kutetea haki zao na za wenzao ni wahuni,tafsiri itakayojengeka miongoni mwa watanzania ni kua hata viongozi wetu ambao wamepita chuoni hapo ni wahuni.

Mungu ibariki Tanzania,mungu ibariki Africa.

No comments: