Monday, March 20, 2006

SUALA LA AJIRA TANZANIA NA FALSAFA YA TECHNICAL KNOW WHO

Tatizo la ajira nchini mwetu liko wazi sana kwa mtu yeyote yule.Hata wale ndugu zangu waliopo nchi za watu nao pia hili wanalitambua fika.Na kuna uwezekano mkubwa kua wote waliopo huko ughaibuni si kutokana na masomo tu,bali pia katika harakati zao za kulipatia ufumbuzi tatizo hili baada ya kukumbana na kero mbalimbali walipokua wakitafuta mahali pa kujipatia riziki baada ya kazi ngumu ya kuperuzi makaratasi shuleni hadi kufikia kilele cha awali cha safari ndefu ya elimu kama vile kutunukiwa shahada ya kwanza au stashahada.

Serikali imekua ikisisitiza kutiliwa mkazo ukuaji wa sekta binafsi kama njia mbadala ya kulitafutia ufumbuzi tatizo la ukosefu wa ajira kwa wananchi wake.Hili bila shaka ni jambo la heri kabisa.Lakini sidhani kama idara mbalimbali za ajira za serikali na sheria zilizopo zinaenda na wakati ili kuhakikisha mambo katika sekta binafsi yanaenda sawa ili kuepukana na matatizo kama vile ya kuajiri watu wasio na uwezo au bila kuzingatia taratibu zilizopo za ajira.

Naandika waraka huu baada ya kupokea malalimiko kutoka kwa rafiki wa karibu wa MAKENE (ambaye ni Binti) juu ya madhila yanayomsibu katika kampuni moja ya binafsi.Na cha kutia hudhuni zaidi ni jambo hili kutokea katika kampuni ya habari ambayo wengi wetu tungetegemea iwe mstari wa mbele katika kulipigia kelele jambo hili.

Suala la ubinafsi,udugu na unani katika sekta ya ajira kwakweli linatia kichefuchefu na liko katika sura mbili nizionazo kwa harakaharaka.Ya kwanza ni ile inayohusu utaratibu mzima wa kumuajiri mtu katika nafasi Fulani na la pili ni lile la upendeleo ulio wazi kazini unaotokana na kujuana kikabila,kindugu au kihusiano na zaidi ni katika masuala ya mapenzi.Nafikiri la mwisho ndilo linaloota mizizi zaidi kwani matokeo yake ni kuharibika kwa kazi.

Nani atabisha kua asilimia kubwa ya wakuu wa idara mbalimbali wana uhusiano wa kimapenzi na makatibu muhtasi wao?Nani atajifanya kusema kua hajui matokeo ya uhusiano huo kua ni kuharibika kwa kazi na kukua kwa dharau kati ya makatibu hao na waajiriwa wengine?Nani ambaye hatambui kua kwasasa asilimia kubwa ya makatibu muhtasi wa wakubwa katika makampuni binafsi ni wale wasiokua na sifa na elimu stahiki kushika nafasi hizo?Nani ambaye hajui kua hawa makatibu muhtasi wamekua na sauti ndani ya mashirika au makampuni binafsi kuliko hata hao wakubwa zao?

Ni majuzi tu nilivyokua Arusha nikimalizia masomo yangu nikiwa katika harakati zangu za kutafuta ajira nikapeleka maombi ya kazi katika shirika moja Mkoani Arusha nikiwa na uhakika wa kuilamba hiyo nafasi.Nikiwa natoka mlangoni mwa ofisi hiyo nikakutana na rafiki yangu tuliyekua tunasoma pamoja shule ya msingi.Katika maongezi yetu nikamueleza lengo la mimi kwenda pale ofisini lakini nilipata hofu nilipomuona ameshtuka na kutikisa kichwa kuonyesha masikitiko yake na ndipo nilipoona kuna umuhimu wa kuhoji kulikoni.Jawabu likawa “huyo Katibu mushtasi wao ana tabia ya kuzichana au kuzichoma moto barua za maombi ya kazi za watu na kutafuta vihiyo wenzake ambao ni jamaa zake kwani uhakika wa wao kupata ajira ni mkubwa kutokana na bosi wao kumuweka kiganjani”!!!!!
Kama nilivyosema hapo juu kuhusu rafiki wa karibu wa Makene aliponipa taarifa za kunyanyaswa na kusengenywa na katibu muhtasi wao nimeona ni busara kushirikishana tena huu uozo ambao wengi wetu tumekua tukishuhudia na tuweze kuchangia juu ya nini kifanyike ili tuokee hali katika hizi idara zianazotegemewa kua kimbilio la watu kujipatia ajira.Nimeambiwa kua imekua ni desturi kwa makatibu muhtasi hao kuwasema kwa mafumbo yanayoshadahishwa na tungo za pwani(Taarabu) wale wafanyakazi wenzao ambao wana chuki binafsi ilhali wakuu wa idara na mashirika husika wanafumbia macho vitendo kama hivi vya kishenzi.Hivi kuna uhalali upi kwa mtu aliyemaliza darasa la saba na asiye na uzoefu hata wa mwaka mmoja kulipwa mshahara maradufu zaidi ya yule mwenye shahada zaidi ya moja na anayeshika nafasi nyeti katika shirika husika????

Hali sasa inazidi kua mbaya kupita maelezo.Kila anayeona tangazo la kazi mahali,kitu cha kwanza anachofanya ni kutafiti na kujua kama ana ndugu,jamaa au rafiki katika sehemu husika ya ajira tarajiwa.Huu utaratibu ndo umekua unazidi kukandamiza wenzangu na mimi wanaotokea TANDAHIMBA kama akina makene kushindwa kupata ajira pindi wamalizapo masomo yao.Hivi sasa vyeti vya taaluma vinakua kigezo cha mwisho kuzingatiwa na badala yake kujuana ndo kumeshika hatamu zaidi.Vikwazo vinakua vingi haswa kwa dada zetu wanaolazimishwa kuziweka taaluma zao kapuni au kwenye pochi na badala yake kutumia miili yake ili kujihakikishia nafasi zilizotangazwa na ambazo nionazo mimi ni kama haki zao.

Nionavyo mimi,ili maisha bora yapatikane kwa kila Mtanzania nadhani utaratibu mzima wa ajira unapaswa kutazamwa upya.AU MWASEMAJE WAKEREKETWA WENZANGU WA GAZETI TANDO?????????????

5 comments:

boniphace said...

Mteru umeniingiza sana katika makala hii hali inayoninyima haki ya kusema niliyokusudia. mPE POLE HUYO BINTI AMBAYE KWA HAPA SIMFAHAMU! Kuna mengi katika mifumo ya maisha ya ajira za Tanzania. Unajua zaidi kuliko mimi maana nikikueleza ni kuumiza mioyo tu ila la msingi kuwa taratibu za ajira zapaswa kuangaliwa upya. Lakini hili la kupenda totoz na ukipata ofisi ya kuajiri unadhani ndiyo fursa ya kufurahisha moyo wako. Haya mbadiliko kama hatapatikana mtu wa kuwadhuru waajiri hawa wakafungwa kwanza itatuchukua karne. Mliopo Bongo nambieni juu ya kashfa ya Lupogo na Leila Sheikh kuhusu udhalilishaji maana yule alisema lakini sijui ilifia wapi, au alipewa kitu kidogo akachuna...Mungu wangu sijui nimalize nini hapa. Baadaye Materu.

Unknown said...

OBAT KUAT SEMPROT PROCOMIL SPRAY
TISSU MAGIC
AFRICA BLACK ANT
CIALIS 20mg
VIAGRA USA
CIALIS 80mg
OBAT PEMBESAR ALAT VITAL
VIMAX PEMBESAR PENIS
KLG PILL
OBAT PEMBESAR PAYUDARA
PUERARIN
OBAT PENGHAPUS TATTO
TATTONOX
OBAT PERANGSANG WANITA
PERANGSANG SERBUK CINA
OPIUM SPRAY
SEX DROPS
AILIDA CANDY
CHEWING GUM
POTENZOL CAIR
OBAT TIDUR WANITA
LIQUID SEX
PEMUTIH WAJAH ALAMI
TENSUNG CREAM
PENGGEMUK BADAN ALAMI
KIANPI PILL GINSHENG
RING PENGGELI
RING PENGGELI VAGINA
SELAPUT DARA BUATAN
SELAPUT DARA PALSU

TOKO OBAT VIMAX

VIMAX CAPSUL CANADA
VIMAX PEMBESAR PENIS

Unknown said...

OBAT KUAT SEMPROT PROCOMIL SPRAY
TISSU MAGIC
AFRICA BLACK ANT
CIALIS 20mg
VIAGRA USA
CIALIS 80mg
OBAT PEMBESAR ALAT VITAL
VIMAX PEMBESAR PENIS
KLG PILL
OBAT PEMBESAR PAYUDARA
PUERARIN
OBAT PENGHAPUS TATTO
TATTONOX
OBAT PERANGSANG WANITA
PERANGSANG SERBUK CINA
OPIUM SPRAY
SEX DROPS
AILIDA CANDY
CHEWING GUM
POTENZOL CAIR
OBAT TIDUR WANITA
LIQUID SEX
PEMUTIH WAJAH ALAMI
TENSUNG CREAM
PENGGEMUK BADAN ALAMI
KIANPI PILL GINSHENG
RING PENGGELI
RING PENGGELI VAGINA
SELAPUT DARA BUATAN
SELAPUT DARA PALSU

TOKO OBAT VIMAX

VIMAX CAPSUL CANADA
VIMAX PEMBESAR PENIS

Unknown said...

VIMAX ASLI
ALAT SEX UNTUK PRIA
VAGINA PANTAT NUNGGING
VAGINA TABUNG
VAGINA SENTER
BONEKA FULL BODY
ALAT SEX UNTUK WANITA
VIBRATOR LIDAH
PENIS TEMPEL GETAR ELEKTRIK
PENIS SILIKON GETAR
PENIS IKAT PINGGANG
BONEKA FULL BODY PRIA
PENIS MUTIARA
VIBRATOR PENGGELI
ALAT PEMBESAR PENIS
VAKUM PEMBESAR PENIS
PRO EXTENDER
ALAT PEMBESAR PAYUDARA
VAKUM PAYUDARA
KRIM PAYUDARA
dr SUSAN CREAM
KONDOM
KONDOM KRISTAL
KONDOM NAGA
KONDOM KAKTUS
MINYAK PEMBESAR PENIS
COBRA OIL
BLACK MAMBA OIL
LINTAH PAPUA
OBAT KANTUNG MATA
OBAT PENGHILANG KANTUNG MATA
OBAT KUAT SEX
KAMAGRA OBAT KUAT CAIR
OBAT KUAT SEMPROT PROCOMIL SPRAY

agaricpro said...

haturnuhun infona....
upami nuju gaduh panyawat jantung bengkak, aya Cara Mengobati Jantung Bengkak secara Alami nyaeta nganggo Obat Herbal AgaricPro. Aos Oge artikel tentang Gejala Jantung Bengkak.

by : www.istiqomahstore.com