Tuesday, March 30, 2010

KUDORORA KWA UFUMBUZI WA MGOGORO WA ZIMBABWE NA HADITH YA MWNAMKE MZINZI KATIKA BIBLIA
Katika Injili ya Yohane 8:1-11 kwenye maandiko matakatifu ya biblia tunapata kisa cha mwanamke mmoja mzinzi aliyepelekwa kwa yesu na mafarisayo na walimu wa sheria kwa lengo la kumjaribu yesu juu ya dhambi ya uzinzi aliyofanya mwanamke yule kwani kwa mujibu wa sheria zao mose aliwaamuru mwanamke kama huyo apigwe mawe hadi kufa. Walipozidi kummuuliza,yesu aliwajibu napenda kunukuu “Mtu asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza kumpiga jiwe”.Kisha akainama tena akawa anaandika ardhini.Wale mafarisayo waliposikia hivyo wakaanza kutoweka mmoja mmoja na kumuacha yesu peke yake na akiwa amesimama palepale.

Kila nikifikiria mgogoro wa Zimbabwe narejea kauli ya Yesu kristo aliyowapa wale wakuu wa sheria na mafarisayo wakiwa katika harakati za kutekeleza dhamira yao ya kumsulubu yule mwanamke mzinzi.Katika makala hii nashindwa kutafuta namna nyingine ya kuwafananisha viongozi wa kiafrika na wale mafarisayo na walimu wa sheria katika jitihada zao teketeke za kuutafutia ufumbuzi wa kudumu mgogoro wa Zimbabwe huku nyumba zao zikiwa chafu kwa kiwango kilekile na wakati mwingine kuuzidi huo wa menzao Mugabe.

Hakuna asiyetambua changamoto mbalimbali zinazoikabili nchi hii iliyo kusini mwa afrika ya jangwa la hasara.Mgogoro wa Zimbabwe kila kukicha unazidi kuchukua sura mpya na madhara ya kibinadamu yanazidi kuwa makubwa. Ukijaribu kuangalia jitihada zinazofanywa na wakuu wa nchi za kiafrika hazilangani na wala kutoa matumaini ya kupatikana suluhu ya haraka katika mgogoro huo ambao unaendelea kugharamu maisha ya wazimbabwe walio wengi na wasio na hatia.

Viongozi wa kiafrika wanatambua kwa undani udhaifu wa mwenzao raisi Mugabe lakini nani mwenye ujasiri wa kukemea ubabaishaji katika serikali yake wakati wenyewe huendekeza ustaarabu wa kizandiki katika dola wanazoziongoza na kuendelea kila siku kusuka mikakati ya kuangamiza demokrasia change ambayo ilianza kupenyeza katika karne ya ishirini ambayo kimsingi ni changamoto mahsusi katika kuchochea maendeleo ya nchi hizi ambazo zinazidi kulowea katika lindi la umaskini mkubwa.

Vyombo vya kikanda katika bara la kiafrika vinabaki kuwa sehemu ya wakubwa kukutana na kuonyeshana ufahari wa kirasilimali wa nchi husika na ukwasi wa watawala huku wakisahau na kuweka kando agenda muhimu za kuwaletea wananchi wake maendeleo na kuimarisha amani.Katika jumuiya ya maendeleo ya kusini mwa Afrika na umoja wa Afrika kuna vyombo mahsusi kwa ajili ya kushughulikia matatizo kama haya ya Zimbabwe.

Vyombo hivi vimebaki kuwa vya kuhifadhiana udhaafu wa wenzao huu wananchi wao wakiendelea kuteseka kila kukicha na kuziacha nchi moja moja kukemea ubabaishaji huo ambazo kimsingi zinakosa nguvu za kukemea uzandiki wa kimadaraka unaowakabili viongozi au wakuu wan chi za kiafrika na hivyo kutoa uhalali wa kuwepo kwao.

Botswana imekua ni nchi pekee kukemea udhaifu huu wa serikali ya Zimbabwe chini ya ubabaishaji dhahiri wa rais Mugabe bila kificho au kuoesha unafiki katika kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo lakini jitihada hizo zilifunikwa na kikao cha wakuu wan chi za kiafrika kilichofanyika misri mwaka jana siku chache baada ya uchaguzi wa marudio wenye utata ambao umoja wa Afrika ulishindwa kuonyesha dhamira ya dhati katika kukemea ubakaji wa demokrasia ulionyeshwa na rais Mugabe.

Nchi za kiafrika zimekuwa vinara wa kubuni mikakati isiyotekelezeka ili kuwashwashi mabwana wakubwa wa nchi za magharibu kuendelea kuzisaidia.Hakuna asiyeamini mkakati uliobuniwa na waafrika wenyewe wakiongozi na wanadiplomasia mahiria kama Thabo Mbeki,Abdulay wade,Olesegun obasanjo wa kufanyia tathmini utekelezezaki wa utawala bora katika dola za kiafrika,maarufu kama APRM ungeshindwa kuwa ni msingi imara wa kuichukulia hatua Zimbabwe ambayo imedhihirika kuzikiuka katika viwango vya kutisha.

Katika hali ya kushangaza rais Mugabe anatoa kauli ya kukanusha kuwa nchi yake haina tatizo la kipindupindu wakati vyombo vya habari vya ndani ya nchi,afrika na dunia vinaripoti ongezeko la tatizo hilo kila kukicha na watu wakendelea kupoteza maisha bila hatia yoyote huku vioongozi wa kiafrika wakiendelea kujigamba mbele ya mataifa ya nje kuwa jukumu la kutatua mgogoro huo liko mkononi mwa waafrika wenyewe wakati kimsingi wamekosa sifa za usafi katika kushughulikia tatizo ambao wao kimsingi wamekua wakiyaendekeza katika nchi zao.

Kueendelea kuvilaumu vyombo vya habari vya kimataifa kuwa vinachochoe au kutia chumvi hali halisi ya matatizo nchini Zimbabwe ni kutaka kukwepesha ukweli ambao kila mtu anaona.Rais Mugabe amekua akitumia hili kama njia ya kujisafisha kwa wananchi wake na kwa viongozi wenzake wa kiafrika ambao kimsingi wameshamchoka ila inabaki dhana ya kutunziana heshima.

Mbinu chafu alizotumia Mugabe katika kujitwalia madaraka na ambazo ameendelea kuzitumia kuiongoza dola ya wanazimbabwa ni mfano tu na kiwakilishi cha uzandiki na ubabaishaji katika nchi mbalimbali za kiafrika hivyo kumfanya apate kiburi cha kukataa shinikizo kutoka kwa nchi nyingine za kiafrika kuingilia mgogoro wake.

Raisi Mugabe ni kama anawauliza viongozi wenzake,ni nani msafi anitupie mawe?Nani ambaye hatendi dhambi anyanyue jiwe anirushie?Nani asiyeiba kura asimame aniambie?Nani asiyekiuka haki za binadamu katika nchi yake?hakika ni mambo mengi yanayofanywa na vioongozi wa nchi za kiafrika ambazo yanarandana na haya yanayotokea Zimbabwe kwasasa nap engine hata kuzidi yanayotokea Zimbabwe.

Pembe zote za afrika iwe kaskazini,kusini,mashariki na magharibi watawala wa nchi zetu wamekuwa wakendesha ubabaishaji kama huu anaoufanya raisi mugabbe na kimsingi hakuna msafi wa kusimama mbele ya hadhara ya kukemea hali hiyo na kuchukua hatua dhidi ya mtawala huyu ambaye anazidi kutia doa ustawi wa demokrasia yetu change ambayo imeanza kuchanua miaka ya tisini.

Umoja wa afrika ulio chini ya rais wa Tanzania mheshiiwa Jakaya Mrisho kiwete iliongoza opereshni ya mafanikio katika kumuondoa madarakani kanali Mohamedi Bakari wa visiwa vya anjuani komoro kwa mafanikio makubwa lakini hatma ya mgogoro wa Zimbabwe hadi sasa haijulikana licha ya kuwa madhara anayosababisha \mugabe kwa kwa wananchi wake ni makubwa zaisdi ya yale aliyokuwa anasabibisha Bakar huko anjuani.

Sina maana kuwa nguvvu za kijeshi ni muafaka katika utatuzi wa mgogoro huoo wa Zimbabwe ila dhamira na utayari wa kutautua mgogoro huo mbona haupo.Nani asiyejua kuwa chanzo cha mgogoro huo ni raisi Mugabe mwenyewe?Nani asiyetambua wananchi wanateseka kwa mambo ambayo kimsingi hawakupaswa kuyakabili?

Viongozi wetu wamekuwa wakijitapa kila kukicha kuwa matataizio ya kiafrika yanapaswa kutatuliwa na waaafrika wenyewe lakini cha kustaajabisha hadi sasa hakuna anayeonyesha nia na uwezo wa kuthibtisha umakini wa kauli hizo kimatendo.Hakuana sababu ya kutafuta umaarufu katika maneno ambayo hayajidhihiriushi katika matendo yenye muelekeo wa kutatua matatizo ya nchi zao.

1 comment:

imanauliya said...

I like it this really good information
Vimax Canada